Sunday, November 4, 2007

Waitara: Sitaki siasa

*Asema ataendelea kuishi Dar es Salaam

Na Happiness Katabazi
MKUU wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) mstaafu, Jenerali George Marwa Waitara (57), amesema hana mpango wa kushiriki katika siasa.

Jenerali Waitara alisema hayo jana kwenye lango la kutokea la Kambi ya Jenerali Twalipo, Mgulani jijini Dar es Salaam, muda mfupi baada ya kusukumwa na maofisa wakuu wanane wenye vyeo vya meja jenerali na brigedia jenerali, kama ishara ya kuagwa rasmi jeshini.

Jenerali Waitara ambaye aliagwa kwa kishindo na heshima zote za kijeshi, alisema hata baada ya kustaafu rasmi Septemba 15, ataendelea kuishi Dar es Salaam kwa kuwa familia yake ina makazi ndani ya jiji.

“Ndiyo nimestaafu lakini nitaendelea kuishi hapa hapa jijini kwa kuwa familia yangu ipo hapa, ila wakati mwingine nitakuwa nikienda Tarime ambako nilizaliwa… ila sihami jijini, nitaendelea kuishi hapa hapa,” alisisitiza Jenerali Waitara, huku akicheka na kusababisha maofisa wa jeshi hilo waliokuwa karibu yake na waandishi wa habari kuangua kicheko pia.

Akijibu mwaswali ya mwandishi wa gazeti hili kwamba ana mpango wa kuingia kwenye medani ya siasa na anatarajia kufanya shughuli gani, alisema kazi anayoijua yeye ni moja, na kuitaja kazi hiyo kuwa ni jeshi.

Alisema hana mpango wa kujitumbukiza kwenye siasa kwa kuwa kazi anayoijua yeye ni jeshi, na kuwa tangu azaliwe hajawahi kufikiria wala kuota ndoto ya kujiunga katika siasa.

Kuhusu shughuli gani ya kumuingizia kipato anayotarajia kuifanya baada ya kustaafu, alisema hadi wakati anastaafu alikuwa hajapanga atafanya shughuli gani na akaongeza kuwa, baada ya mapumziko ataangalia na kushauriana na ndugu na jamaa zake kuhusu shughuli atakayoifanya.

Mkuu mpya wa JWTZ, Jenerali Davis Mwamunyage, alimkabidhi mstaafu huyo kitambulisho cha kustaafu, ikiwa ni ishara ya kumuaga na Waitara naye alimkabidhi kitambulisho chake cha kazi, alichokuwa akikitumia kabla ya kustaafu.

“Leo nina furaha kubwa sana ya kukukabidhi hati hii ambayo utaitumia baada ya kustaafu… na ninakukabidhi hati hii kwa niaba ya JWTZ kama ishara ya kutambua na kuheshimu utumishi ndani ya jeshi hili… hongera sana na nina furaha sana kuona unastaafu kwa amani na kuliacha jeshi likiwa imara,” alisema Jenerali Mwamunyange.

“Nami nakukabidhi kitambulisho changu ambacho nilikuwa nikitumia kabla ya kustaafu kazi ya jeshi kama ishara ya kitambulisho hicho kwisha muda wake,” alisema Jenerali mstaafu Waitara.

Sherehe za kuagwa kwa mstaafu huyo zilianza saa 2:30 asubuhi katika Kambi ya Jenerali Twalipo, Mgulani kwa gwaride lililokuwa na gadi sita.

Awali, gadi hizo zilifanya gwaride la kumkaribisha Mkuu mpya wa jeshi hilo, Jenerali Mwamunyange, ambaye aliapishwa Jumamosi iliyopita na Amiri Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Kikwete, na kisha kupita mbele kwa ukakamavu na kisha kutoa heshima kwa mwendo wa pole na haraka.

Baada ya kumaliza kutoa heshima, gwaride hilo lililokuwa likiongozwa na Kanali Raphael Mataba, liliumba umbo la Omega ikiwa ni ishara ya utumishi wa mwisho wa Waitara katika jeshi hilo.

Baada ya tukio hilo kumalizika, Waitara alipakiwa kwenye gari maalumu la wazi lililokuwa lilisukumwa na maofisa wa jeshi taratibu. Maofisa hao waliongozwa na mameja jenerali wawili. Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Martin Madatta na Meja Jenerali Sylvester Rioba.

Wengine sita waliomsukuma ni wenye vyeo vya brigedia jenerali, Said S. Omar ambaye ni Mkuu wa Kikosi cha Wanamaji (Navy), Seni Hinda, Charles Makakala, Rasul Kilonzo, Kamaro Ileti na Albert Balati.

Sherehe hizo zilihudhuriwa na Kaimu Kamishna Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, Aziza Murhsal, Waziri wa Fedha, Zakia Meghji, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Profesa Juma Kapuya, majenerali wastaafu, waambata wa kijeshi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini na wananchi wa kawaida.

Wakati huo huo, maofisa na askari wa kawaida walimmwagia sifa Waitara wakimtaja kama kiongozi imara aliyeliongoza jeshi katika misingi ya haki na maadili mema.

Waitara alistaafu rasmi Septemba 15 mwaka huu. Alizaliwa Septemba 15 mwaka 1950 katika Kijiji cha Itirya, Wilaya ya Tarime, mkoani Mara. Alimaliza masomo yake ya Sekondari katika Shule ya Sekondari ya Minaki mwaka 1969.

Alijiunga rasmi na jeshi hilo mwaka 1970 akiwa ofisa mwanafunzi, na alipata kamisheni mwaka 1971, na kuhudhuria mafunzo mbalimbali ya kijeshi.

Mwaka 1978, katika vita ya Tanzania na Uganda, Waitara alikuwa miongoni mwa makamanda walioongoza vikosi katika vita hiyo.

Wakuu wa majeshi wengine waliomtangulia Waitara ni Sam Hagai, Mrisho Sarakikya, marehemu Abdallah Twalipo, David Musuguri, Ernest Mwita Kiaro na Robert Mboma.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima,Septemba 18,mwaka 2007

TSPCA yapinga wanyama kuuawa

Ddc

Na Mobini Sarya

HATIMAYE Shirika la Maendeleo Mkoa wa Dar es salaam,(DDC) limetoa taarifa kuwa Mkandarasi aliyekuwa anajenga vibanda vya biashara eneo la DDC Kariakoo anamkataba unaomwezesha kujenga na kupangisha (BOT).

Taarifa hiyo inaonekana kuhitimisha mvutano uliokuwa unaendelea chinichini kuhusu ni nani anaeyestahili kupangisha na kuendesha eneo hilo lenye vibanda 64, kati ya Mkandarasi ambaye ni Kampuni ya ujenzi Nimeta Construction iliyojenga na Shirika la DDC.

Kampuni ya Nimeta ilipewa Tenda ya ujenzi huo ulionza Mei Mwaka huu baada ya wafanyabiashara 52 kuoondolewa hapo kwa maelezo kuwa eneo baada ya ujenzi kukamilika watalejeshwa hatua ambayo walipinga na kufikia hatua ya kuchangishana pesa ili wajenge wenyewe wakidai kuwa mkandarasi akijenga atawanyima nafasi ya biashara.

Akizungumza na Tanzania Daima Mwishoni Mwaka wiki Meneja Utumishi wa DDC, Shabani Juma alisema kuwa kasasa vibanda hivyo vimekwishakamilika wanachosubiri, mkandarasi huyo atangaze tenda kwenye vyombo vya habari ili anayehotaji aombe.

Maelezo hayo yanapingana na maelezo ya awali yaliyokuwa yanatolewa na Meneja wa Shirika hilo Mhando Muya alipokua akielezea ujenzi wa Vibanda hivyo na yanakuwa kama pigo kwa wale wafanyabiashara walioondolewa hapo kwani inavyoonekana Mkataba wa BOT utakuwa unampa uwezo mwekezaji kupangisha mpangaji anayemtaka yeye.

Ingawa Mhando mara zote amekuwa akisisitiza kuwa mkandarasi anajenga tu nakujiondoa wao wanawapangisha, wakiwapa kipaumbele wafanyabiashara walioondolewa, hata hivyo baada ya taarifa hiyo kutolewa hakuweza kupatika mara moja kuelezea upi upi msimamo wapamoja kuhusiana.

na Mobini Sarya

manispaa ya Ilala yakubali umbwa wote wachanjwe bure

MANISPAA ya Ilala imekubali ombi la Chama cha kuzuia ukatili kwa wanyama (TSPCA), ambacho kilimwadikia barua Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kikiomba asitishe zoezi la kuwasaka na kuwaua wanyama wanaofungwa ambao watabainika wakizurura mitaani bila kuwa na chanjo chanjo ya kichaa.

Akizungumza na Tanzania Daima Ofisini kwake katibu mtendaji wa chama hicho, Johari Gessan alisema kuwa baada ya kukubaliwa sasa wataanza kama awali manispaa hiyo ilikuwa ikisimamia zoezi la chanjo kwa umakini baada ya hapo watapita nyumba kwa nyumba kuwachanja wanyama wote.
Pia Gessan amesema zoezi hilo ambalo litaanza jumatatu watakuwa wanagawa cheni kwa wamiliki wa wanyama hao kuwafungia wanyama hao wasizurure, kwa wanyama ambao watabainika hawana mmilki watawakamata na kuwafundisha tabia njema na kumpa mtu yeyote atakayetaka huku waakimjengea kibanda bure.
“Baada ya ombi letu kukubaliwa tutaanza jumatau kupita nyumba kwa nyuma kuwahamasisha watu wajitokeze kuchanja wanyama wao, tutashirikiana na maaafisa mifugo wa kata, zoezi litakaloenda sambamba na kugwa cheni pamoja na kuwahesabau wanyama wote”alisema Gessan.
Katika barua waliyokuwa wamemwandikia mkurugenzi wa manispaa hiyo ilikuwa inanukuu tangazo lililotolewa Oktoba 10 mwaka huu lililokuwa likitaarifu kuwapo kwa msako wa kuwaua mbwa, paka na nyani ambao hawajapata chanjo za kichaa.
Gessan, alisema badala yake kinatoa pendekezo la kufanya kampeni za muda mrefu na za kudumu kwa wananchi wote kuhusu utunzaji wa mifugo na kuwepo kwa huduma zao za msingi, kazi ambayo tayari wamekwishaianza katika ngazi ya kata na serikali na serikali za mitaa wakianzia na Mkoa wa Dar es Salaam.
TSPCA kimeomba wananchi kutoa taarifa pale wanapoona wanyama wanateswa na kunyanyaswa bila sababu ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria kwani ni wanaharakati pekee wanaotetea haki za wanyama kisheria.



juu

Friday, November 2, 2007

MAPINDUZI KATIKA TIMU YA SIMBA

ENYEKITI wa zamani wa muda aliyewahi kuiongoza timu ya Simba ya jijini Dar es Salaam, Michael Wambura na kiongozi wa kundi la Friends of Simba Evance Aveva, wanatarajiwa kuiongoza klabu hiyo katika mapinduzi yanayotarajiwa kufanyika Jumapili.

Habari za uhakika zilizopatikana ndani ya klabu zinasema kwamba mkutano wa dharula ambao unamlenga Mwenyekiti wa klabu hiyo Hassan Dalali ‘Field Marshal’ anatarajiwa kupinduliwa na nafasi yake kuchukuliwa na Wambura au Aveva kwa madai ya timu kufanya vibaya.

Mtoa habari huyo anasema kwamba baada ya kuona timu inaendelea kufanya vibaya katika Ligi ya Vodacom inayoendelea katika viwanja mbalimbali, Dalali ameshtuka na kupinga mkutano kwa nguvu zote .

Mkutano huo uliotangazwa hivi karibuni na Kaimu Katibu Mkuu wa Simba Said Rubeya ‘Seydou’ kuitisha mkutano wa Wanachama kujadili mwenendo mbaya wa timu yao katika Ligi Kuu.

Akizungumzia kuhusu mkutano huo Dalali, alisema kuwa mkutano ni batili kikatiba kwa sababu wanachama tayari walishafanya mikutano miwili yaani wa Aprili na Agosti, hivyo mkutano uliobaki utafanyika Desemba ili kuzungumzia mapato na matumizi.

Dalali alisema kuwa haogopi mapinduzi kwani katika maisha yake hajali kabisa mambo hayo.

Wakati hali ikiwa hivyo, baadhi ya Wanachama wa Simba jana walifika kwenye ofisi za Sayari na kusema kuwa wanaunga mkono kauli ya Seydou kufanya mkutano Jumapili unaotarajiwa kufanyika makao makuu ya klabu hiyo.

Wanachama hao Khamis Ng’ombo mwenye kadi 0113, Fatuma Mohammed 1880, Zintanga Maji 3305 na Mashaka Ally 0770, kwa pamoja walisema kuwa Wanachama wajitokeze kwa wingi kwenye mkutano huo utakaoanza saa 4:00 asubuhi.

Akizungumza kwa niaba ya wanachama Ng’ombo alisema kuwa mkutano huo utazungumzia matatizo baina ya timu kufanya vibaya kwani waliwatembelea wachezaji kambini waliwaambia kuwa uwezo wanao lakini wanamatatizo na viongozi wao.

Alisema kuwa viongozi hawawatimizii mahitaji muhimu , hivyo tunaomba siku hiyo wanachama wajitokeze kwa wingi kujadili masuala mbalimbali ya klabu ikiwamo mikataba ya wachezaji inaisha mwezi huu.

“Sisi wanachama matatizo ya klabu yanatakiwa kujadiliwa na viongozi na wanachama ili kuinusuru klabu pamoja na timu hivyo kisheria tunayohaki ya kuitisha mkutano huo ambao tunashukuru Seydou ameona mbali na kuamua kuitisha mkutano,” alisema Ng’ombo.

Alisema kuwa wakati waliwatembelea wachezaji ilikuwa ni kabla ya mechi na watani wao Yanga waliwaahidi kuwa watashinda lakini walisema wana matatizo kitendo ambacho walikifanya kwani waliishinda Yanga bao 1-0.

Ng’ombo alisema kuwa timu yao wanaamini iko imara hivyo wamesisitiza wanachama kufika kwa wingi ili kuweza kuinusuru klabu hiyo wasisikilize maneno ya Dalali kwani yeye ni Msimamizi tu , mtendaji ni katibu ambaye katiba inamruhusu kuitisha mkutano.

Mwisho .

Monday, October 29, 2007

Alichokisema butiku kwa upanambele ya waandishi wa habari maelezo

Butiku
NA m S

WIKI iliyopita Mwanasiasa Mkongwe wa Chama Chama Mapinduzi CCM, Joseph Butiku ambaye pia alikuwa msaidizi wa Karibu wa Rais wa Kwanza Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarag Nyerere, alijtokeza mbele ya waandishi wa habari na kusema maneno makuu yanayoashiria mstakabali w a taifa hili.

Ni kiwa miongoni mwa waandishi tuliohudhuria kikao hicho ukumbi wa idara ya habari MAELEZO nimeona ni vema nikaandika kwa kina aliochokuwa anakilenga katika mazungumzo yake, wakati alipoanza kujitambulisha kama Raia Mwaminifu na Mwanachama mwanzilishi wa CCM aliyejitokeza bila kutumwa na Tasisi ya Mwalimu Nyerere “sikuja kama nimetumwa na mfuko hapana nimekuja kama mimi” alisema.

Aliendelea ‘mimi ni bubu huwa sipendi kusema maneno haya nah ii ni kutokana na jinsi tulivyolelelewa kimaadili, leo nimeamua kusema kutokana na ujmbe unaotolewa kwenye vyombo vya habari ambao unahusu viongozi,sisemi kwa ushabiki au kama au kama mpinzani au mtu asiye na adabu nayasema haya kwa dhati kabisa na pale ninapo taja majina sio kama mpuuzi ila nazingatia maadili ya uongozi.

Mwanasiasa huyo alisema kuwa ameamua kujitokeza baada ya kuona kelele za rushwa zinazidi kuwa nyingi, usimamizi mbovu wa maliasili zetu ,umasikini kuzidi kuongezeka ,mali zina potea hovyo na wanaopiga kelele ni sisi wenyewe watanzania.

“kelele hizo zinahusu viongozi na uongozi wan chi, sisi sote kila mmoja anakichwa kinachomuongoza kwa hiyo wote ni viongozi ,matatizo haya yanayoizungumzwa ni yetu sote” Alisema huku akionyesha Katiba ya kwanza iliyoandikwa wakati wa uhuru na iliyotambua kuwepo serikali ya Muungano wa Tanzania katika hiyo ilikuwa na mambo manne ya aliyoyasoma ambayo ni;vyombo vyote vya kiserikali lazima vieleweke kwa wananchi ,Mamlaka inayoongoza itoshe katika kusimamia shughuli, Bunge lijitegemee na mwisho alisema lazima utawala wa kisheria ukubaliwe.

Na ndivyo inapaswa kutendwa hata Rais anaapa kuilinda katiba anapochaguliwa pia anaapa kuwa ataongoza bila upendeleo wowote ikiwemo kuwapendelea ndugu zake na kwa upande wa chama chama cha Mapinduzi katiba inasema hvyo ,hizi katiba zote mbili zinatupa uhuru wa kushughulika na mambo yetu kwa mjibu wa katiba.

Butiku anakumbusha kuwa wakati wachama kimoja kiongozi alikuwa anaapa kuwa hatapokea wala kutoa rushwa leo imepita zaidi ya miaka 40 tangu iandikwe katiba ya mwaka 1962 iliyoasisiwa na Mwalimu Nyerere ,Maadili yameporomoka na Rushwa hapa nchini sasa imekuwa kama ugonjwa wa UKIMWI usio na tiba wakati katiba zote zinazuia.

Anasema kuwa Rushwa ipo kwa sababu viongozi wakuu hawasimamii ipasavyo maadili ipasavyo ,wangeyafuata na kuheshimu katiba ya nchi na chama haya yote yanayozungumzwa na kupigiwa kelele yasingetokea hivi sasa.

Kwa mtazamo wake anaona Suala la Rushwa linachakigiwa kwa kiasi kikubwa na wananchi kutokuwa makini na Serikali yao “sisi wananchi tumekuwa kama makinda ya ndege yanayoachama mdomo yawekewe chakula,tunaachama midomo watawala wanatuwekewa mdomoni”anasema hiyo kauli aliwahi kuitoa akiwa Kongozi Singida.

Akifafanua kauli yake hiyo alitolea mfano kwenye jimbo analotokea la Musoma Vijijini Ambapo mbunge wake aliwafanyia maendeleo wananchi wake lakini kilipofika kipindi cha uchaguzi mwingine akaja mpiunzani wake yule mbunge akawaambia wananchi mimi nimewasaidia maendeleo na nitaendelea kuwasaidia nichagueni lakini wananchi hawakujali hilo wakamlazimisha kutoa rushwa.

Hali hiyo ilimfanya Butiku amfuate mbunge huyo kumuuliza swala hilo kama alitoa Rushwa akajibiwa kwamba wananchi walimlazimisha wanakwenda hadi nyumbani kwake ikabidi awawekee pesa mezani wagawane, kwa mfano huo anaeleza unajionyesha jinsi maadili yalivyokwisha hata kwa wananchi.

Anasisistiza kuwa viongozi wapo wanaotoa Rushwa ndani ya CCM hakuna anayeweza kupinga hilo, na mtu yeyote akishakuwa kama Kinda atawezaje kuwa Kiongozi au mwanchi mwema? Hata akichaguliwa kuwa Waziri atabaki na ubovu wake huohuo ndio maana Rushwa inadhidi kwa viongozi kutokana na tabaka wanalotokea.

Hali hiyo imekuwepo tangu Uhuru kwani kilikuwa ni kipindi kifupi tu tangu Rais wa Kwanza Mwalimu Nyerere akabidhiwe madaraka na Kuunda Serikali wakati Waziri wake akatuhumiwa kula Rushwa Mwalimu akaamuru atandikwe viboko na kutupwa Jela lakini mwingine aliyehushwa naye akaachwa bila maelezo tangu siku hiyo kulindana kukaanza.

Anasema kuwa tatizo la Rushwa ndani ya Chama cha Mapinduzi na halikuanza leo kwani hata serikali ya awamu ya pili lilikwepo ikafikia hatua ikaundwa tume ya kulichunguza na ikapeleka taarifa kuwa CCM yote inanuka Rushwa, kufuatia taarifa hiyo Rais akaamuru watuhumiwa wakajieleze kwenye mkutano lakini Waziri Mmoja akagoma.

Kutokana na Orodha iliyotajwa Waziri Mkuu wa wakati huo (sasa)Jaji Joseph Sinde Warioba akamshauri Rais Alhassan Mwini avunje Baraza lote kwani kama mawaziri wangejieleza ingekuwa aibu kubwa baraza zima kutuhumiwa kwa Rushwa likaundwa jipya mawaziri saba wakaachwa nje.